Kuna aina nyingi za kamba ambazo mimi binafsi nazijua. Kuna
kamba za ujenzi, kutengenezea fito, kuanikia nguo, kuvutia magari, kufugia
mizigo na aina nyingine ambazo wewe unazifahamu.
Katika ulimwengu wa roho kuna aina tatu (3) za kamba nazo ni
Kamba za Mungu ambazo hutoka mbinguni, aina ya pili ni kamba za mwanadamu
ambazo hutoka duniani, na ya tatu ni kamba za shetani ambazo hutoka kwa shetani
mwenyewe.
Na vyanzo vya kamba hizi zote hutoka kwenye madhabau. Za Mungu
hutoka kwenye madhabau ya Mungu ambazo hutoa kwa wanadamu ili wazitumie. Zile
za shetani ndizo humpa nguvu shetani kuweza kuwakamata wanadamu vizuri kwa
kupitia dhambi wazitendazo hapa duniani.
Kitabu cha Waamuzi
6:22 kinasema Gideoni akanona ya kuwa ni malaika wa Bwana; Gidioni akasema,
Ole wangu, Ee Bwana Mungu! Kwa kuwa nimemowna Bwana uso kwa uso. Hata unatakiwa
kama unataka kumuona Mungu uso kwa uso unachotakiwa kufanya kwanza ni kuvunja
utaratibu wako ambao ulikuwa umeuzoea tangu hapo mwanzo na ndipo ujenge na
Mungu.
Sasa naona tuangalie hizo madhabau ambazo humuumiza mwanadamu
kwa njia moja au nyingine kupitia kwa shetani. Ziko saba nazo ni Madhabau ya
dhambi, wasio haki, mauti, kuzimu, mateso, ukiwa, ubatili, nira, wanadamu,
kupimia, na fedha.
Tuanze kuangalia madhabau ya dhambi ni kwa kamba za shetani
hutumia kumvuta mtu kwa urahisi kutokana na dhambi anazotenda na akisha mvuta
huyo mtu huanza kumfunga mafundo, mitego ya aina mbalimbali ikiwa ni pamoja ya
afya ya mtu, fedha katika kufunga kipato chake, au hata katika biashara zake
iwapo mtu huyo atakuwa ameangukia dhambini.
Nayo Mithali 5:22
inasema, Maovu yake yeye yatampata mdhalimu, Naye atashikwa kwa kamba za dhambi
zake. Je wewe kamba za dhambi zako au za wazazi wako hazijakushika mwenyewe ndiyo maana unapatwa
na mateso hayo yote. Unachotakiwa kufanya ni kufanya toba ya kweli ambayo
itakuweka huru na kamba hiyo ya dhambi.
Ya pilini kamba za wasiohaki. Tuone Zaburi
119:61 inasema; Kamba za wasio haki zimenifungako, Sikuisahau sheria yako. Hapa wanazungumziwa wale ambao hupenda
kuwakatisha wenzao tamaa wakati wa kumfuata Mungu. Huwapa maneno ya kebehi,
kejeli na hata dharamu ya kuwa matatizo yote hayoi unayoyapata kama Mungu wako
yupo si akuondolee. Lakini hawajui kuwa kama mtu anataka kumfuata Mungu lazima
apitie kwenye mateso. Dhahabu haiwezi kuwa nzuri hadi ipitishwe kwenye
moto. Na kama ukikataa kupishwa kwenye
mtoto utawezaje kung’aa?
Kamba za tatu ni za Mauti. Mauti hubeba nguvu ya kifo, pia
hupoteza kabisa uhai wa kila kitu ikifanyacho lazima kife. Ikiwa mtu ameanzisha
biashara huanza vizuri lakini mwisho wake huishia kufilisika kwa biashara yako.
Pia katika kazi unaweza ukafanya kazi zako vizuri lakini kabla umri wako wa
kustaafu haujafika unaweza ukaipoteza hiyo kazi na ukaendelea hivyo maisha yako
yote.
Vile vile, inaweza kuathiri katika uzao, kama mtu anakuwa ana
kipawa cha kitu Fulani ambacho mara nyingi akifanya jambo fulani watu
hushangazwa na hicho kipwa lakini inatokea tu ghafla kipawa hicho kinapotea au
kuzimika kama mshumaa unavyozimika ukiwekwa kwenye upepo.
Zaburi 18:4 inasema,
Kamba za mauti zilinizunguka, Mafuriko ya uovu yakanitia hofu. Kamba za mauti
hizo huweza kusababishwa na magonjwa, hofu, njaa, woga, kutafuta mali kwa njia
zisizo halali na vitu vingine vingi.
Aina nyingine ya nne ni Kamba za kuzimu. Zaburi 18:5 inasema, Kamba za kuzimu zilinizunguka,
Mitego ya mauti ikanikabili. Hapa tunaona jinsi kamba za kuzimu
zinavyoshirikiana karibu sana na kamba za mauti ili kamba za mauti ikisha mmeza
mtu humpa kwenzake kamba za kuzimu kumalizia kazi zake. Hivyo unaona jinsi
shetani alivyopanga watu wake kwa ushirikiano mkubwa kuwadhuru wanadamu.
Angalia jinsi Isaya
14:9 inasema; Kuzimu chini kumetaharuki kwa ajili yako, Ili kukulaki
utakapokula; Huwaamsha waliokufa kwa ajili yako, Naam, walio wakuu wote wa
dunia; Huwainua wafalme wote wa mataifa, Watoke katika viti vyao vya enzi. Hapa
tunaona kuwa mtu asiye haki anapokufa kuzimu hutaaruki ikimpokea kwa shangwe
kwa mwenzao amefika je wewe unataka nayo kuzimu itaaruki kwa kufa na dhambi
zako unazozikumbatia? Muda bado fanya toba kweli.
Kamba za tano ni za Mateso. Ayubu 36:8 inasema, Nao wakifungwa kwa pingu, Wakitwaliwa
kwa kamba za mateso; watu wengi hapa ndipo walipokuwa wamenaswa na kamba hii ya
mateso kuanzia jua linapochomoza hadi pale linapozama ni mateso mtindo mmoja
hakua ahueni hata kidogo. Dalili za kamba hiii ya mateso ni utamuona mtu wa
aina hiyo hana raha katika maisha yake anayoishi, kazini anapofanya kazi,
majirani zake wanaomzunguka na hata
kwenye familia yake ni vurugu mtindo mmoja.
Hizi kamba za mateso zina vitu saba (7). Tuone Ayubu 5:16-27 lakini tuone ule mstari
wa Ayubu 5:19 unasema, Yeye
atakuokoa na mateso sita; Naam, hata katika saba hapanba uovu utakaokugusa. Katika
kamba hizi ambazo zinakuandama katika maisha yako Bwana anauwezo kwa kukuokoa
katika vitu hivyo saba.
Cha kwanza ni kukuokoa katika kamba za mauti na njaa. Unaweza
kuzongwa na njaa kwa muda mrefu ambapo kama njaa ikiwa ni kali kupita kiasi
huweza kusababisha mtu kupoteza maisha Mungu anaweza akakukuepusha na baa hilo
la njaa lisikupate likaishia njiani.
Kitu cha pili wanakuokoa na nguvu za upanga, wa tatu ni
mapigo ya ulimi, wan ne ni aina zozote za maangamizo ambayo unayajua yanaweza
kukudhuru kwa njia moja au nyingine uhai, afya, uchumi wako na vitu vingine
vingine. Pia vitu kingine cha tano ni huponjwa na wanyama wakali, cha sita
huponywa na laana ya uchache pia cha saba ni vifo vya mapema.
Kamba ya sita ni kamba za Ukimwa. Hapa asilimia kubwa
huwapata wale watu wandoa ambao kati ya mwenza mmoja ameendea kwa mganga na
kufanyiwa dawa huko ya kupendwa zaidi. Hapa utaona kuwa mwanaume au mwanamke
akiingia ngani huona kama vile ameingia chooni anaona kuwa hapafai kukaa ingawa
ni nyumbani kwake.
Lakini anapotoka nje hujioni kuwa afadhali ya kukaa nje
kuliko kukaa ndani. Isaya 34:11
inasema, Kaati ya nungu wataimiliki, bundi na kunguru watakaa huko, naye
atanyosha juu yake kamba ya ukiwa na timanzi ya utupu.
Kamba ya saba ni Kamba za Ubatili Isaya 5:18 inasema, Ole wao wavutao uovu kwa kamba za ubatili, na
dhambi kama kwa kamba za gari! hapa
inawapa onyo wale wanaovuta sigara ana aina nyingine yeyote ya kileo hicho.
Kwamba yeyote anayevuta sigara na aina yeyote ya kileo hicho huvuta uovu.
Kamba ya nane ni Kamba za Nira. Isaya 58:6, inasema, Je,
saumu niliyoichagua, siyo ya namna hii? Kufungua vifungo vya uovu, kuzilegeza
kamba za nira, kuwaacha huru walioonewa, na kwamba mvunje kila nira? Mfano wa
kamba hizi ni kwa wale ambao wakulia wanautumia au kama si mkulima umeshawahi
kuona jinsi ng’ombe wanaofanya kazi ya kulima hufungwa nira kwenye shingo zao.
Hapa tunaona kama hizo nira za hao ng’ombe zisipofungwa vizuri hawataweza
kulima.
Tunoana katika 2
Wakorinto 6:14 inatuonya kuwa tusifungiwe nira na wale wasioamini sawasawa
na kuenenda na marafiki ambao ni wevi, wanzinzi, washerati, waongo, wachawi na
wangine wengi ambao ni machukizo mbele za Mungu, hatuwezi kuchanganya nuru na
gizi kwa sababu panapo nuru giza haikai.
Kamba ya tisa ni Kamba za Mwanadamu; Hosea 11:4 inasema, naliwavuta kwa kamba za kibinadamu, kwa mafungo
ya upendo; nami nalikuwa kwao kama hao waondoao kongwa tayani mwao, nikaandika
chakula mbele yao.
Hizi kamba za wanadamu humsababishia mtu kumwa mwoga na hata
kama ulikuwa mtu ulimpa kitu kwa kutimia mikono yako kwa hiari yako mwenyewe
kwa moyo safi lakini mtu yule uliyempa kile kitu akaenda akanda kwa mganga au
kama ana yale maarifa ya kishetani anaenda kwenye kaburi na kuzika kile kitu
ulichompa kwa mikono yako mwenyewe kwa hiyo atakuwa amekufunga kila kitu katika
maisha yako. Hutaweza kufanikiwa katika jambo lolote maana kaburi halisemi na
vitu vyako vyote utakavyofanya kuanzia hapo havitafanikiwa.
Kamba ya kumi ni Kamba za Kipimo. Hizi kamba ambazo mtu
anakuchokoza kwa njia yeyote ile ili ufanye uovu. Hapa hutumia njia nyingi
anaweza kukujaribu katika uwezo wako kazini, kujitoa kwako katika kazi za Mungu
na hata za kijamii. Atakupa jambo ulifanye ukifanikiwa hukasirika la
usipofanikiwa hapo ndipo huanza kuivuta hiyo kamba yako ya kipimo kwa lile kosa
ulilofanya kwa wakati ule. Unatakiwa kujiangalia sana kwa huyo mtu uliyekuwa
naye karibu je, nirafiki wa kweli au ni kamba ya kipimo chao?
Kamba kumi na mmoja ni kamba za Fedha; hapa kuna zile kamba
za chuma ulete ambapo kila hela unayopata kutokana na kazi unayofanya hufanyii
kazi yeyote huisha tu bila kufanya kitu cha maana. Unaweza ukatumia katika
anasa na uchawi, uganga, matambiko, makafara, kutoa mimba, na vitu vingine
vingi ambavyo utatumia fedha yako. Mhubiri
12:6 inasema, Kabla haijakatika kamba ya fedha, au kuvunjwa bakuli la
dhahabu; Au mtungi kuvunjika kisimani; Au gurudumu kuvunjika birikani. Tunakumbushwa kuwa je kamba zetu za fedha
tumeziunganisha wapi wa waganga, madhabau gani, matambiko, ulevi, uzinzi,
uasherati, anasa, uuaji na vitu vingine vingi.
Watu wengi hujilaumu kuwa nilikuwa na fedha nyingi lakini
sasa sina je, hujiulizi kamba yako ya fedha aliyokupa Mungu umeiunganisha wapi?
Ukisha kumbuka kuwa umeiunganisha sio mahali pake, hujachelewa unatakiwa kuomba
Mungu toba ya kweli na kurejeza kamba yako ya fedha.
Jinsi ya kuharibu hizo kamba zote 11 nilizozitaja hapo juu.
Unachotakiwa kuzingatia kwanza ni kufanya maombi ya vita Waefeso 6:10. Tumia malaika, damu ya Yesu, Maneno ya kinabii, Uwe
mtu wa imani, tumia malaika kwa upanga ukatao kuwili. Kumbuka kabla ya kuanza
maombi hayo ya vita jikague kwanza wewe ukoje uko safi au una mawaa? Na kama
una mawaa huri magotini uombe toba ya kweli ili upate kibali cha kukata hizo
kamba kumi na moja.
NGUVU
ULIOKUWA NAYO KATIKA KUMFUATA MUNGU
KUREJEZA NGUVU
ZA UJANA ZILIZOPOTEA
Mara nyingi mtoto anapozaliwa huwa kunafuraha sana katika ile
familia ambayo wamepata mtoto. Pia ndugu jamaa na marafiki kutoka sehemu
mbalimbali huja kumuona mtoto aliyezaliwa wakiwa wamebeba zawadi mbalimbali, hali
kila mmoja hawezi kuja kwa mtoto akiwa mikono mitupu.
Pia uzee nao hufurahiwa sana kwa kuwa mtu huyo huwa na busara
na hekimka za kutoa ushauri mbalimbali. Lakini umri wa vijana wengi huwa na
maisha yenye uchungu ambapo mwisho wake huishia kubaya. Lakini yupo mmoja
awezae kurejeza ujana wako.
Tuone anasemaje, Zaburi
103:4-5. Auokomboa uhai wako na kaburi. Aushibisha mema uzee wako, ujana
wako ukarejezwa kama tai. Je, wewe
kijana ujana wako umeupotezea wapi? Mpaka hivi sasa unasumbuka kwa mateso
ambayo yanakuandama siku hadi siku, hadi umekata tamaa ya maisha ya ujana wako?
Tuangalie huyu ndege tai ambaye akiona kuwa amekuwa mzee
huenda sehemu ya mbali sana kwenye pango ambapo hujificha huko huku akinyonyoa
manyoya yake ya mwili mzima. Hapo huanza kuota manyoya mengine mapya na yakisha
kamilika yote hutoka kwenye lile pango na kuanza maisha mengine upya.
Je, wewe umeisha ingia pangoni kuweza kunyonyoa hayo manyoya
yako ambayo yaliyokufanya upoteze uhai wa ujana wako? Hujachelewa Yesu
anakusubiri uje pangoni ili aweze kukukarabati ili ukitoka uwe mpya katika
ulimwengu huu.
Wengi wetu tuliuza ujana wetu kwa waganga, uchawi, uasherati,
uzinzi, maangano, matambiko, ibada za sanamu, ulevi, wizi, uongo na vitu
vingine vingi ambayo havimpendezi Mungu. Hivi vyote vilivyopoteza ujana wako ni vitu
ambavyo shetani alikutenda kwa hili ili uwe mfuasi wake.
Hujachelewa unachotakiwa kufanya ni kudai miaka yako kwa
muumba wako ambaye ni Baba yetu wa Mbinguni; ila tusisahau kuwa Mungu wetu ana
kanuni zake ambazo yeye husimamia kwenye kweli, haki na hukumu.
Je, sisi tu wa kweli mbele za Mungu na ndugu zetu au
tunampenda Mungu tusiyemuona na kumchukia ndugu ambaye tupo naye. Tuone Yoeli
2:21-26. Lakini hapa tuangalie zaidi ule mstari wa Yoeli 3:25,26 unasema: Nami nitawarudishia hiyo miaka iliyoliwa na
nzige, na parare, na madumadu, na tunutu, jeshi langu kubwa nililolituma kati
yenu. Nanyi mtakula chakula tele na kushiba, na kulihimidi jina la Bwana Mungu
wenu, aliyewatendea mambo ya ajabu; na watu wangu hawatatahayari kamwe.
Tujiulize, ni kwa nini mtu huanza na maisha mazuri na kisha
mwisho wa maisha yake huishia maisha ya tabu na dhiki kuu? Ni nini
kinachosababisha mtu kuwa na maisha ya aina hii. Pia Mungu husababisha mtu
kupatwa na matatizo hayo kwa sababu mara nyingi mtu anapopata neema na utajiri
huwa wanamsahau aliyewapa na huanza kuenda kwenye miungu mingine ambayo ni
chukizo mbele zake yeye aliyekupa.
Na hapo shetani huwa na ushawishi mkubwa wa kuwahadaa wana wa
Mungu kwa hila ambazo hutumia ikiwa nia pamoja na hucheza na afya, uchumi,
elimu, ufahamu, nyota, uzao na vitu vingine vingi ambayo anajua hapo akigusa
tu, huyu mwanadamu lazima atakengeuka na kuenda upande mwingine na hapo ndipo
yeye huanza kuwinda nyendo za mwanadamu usiku na mchana na akisha mpata hapo kunakuwa
hakuna tena amani katika familia, kazini, shuleni na hata sehemu yeyote ile
ambayo upo.
Asilimia kubwa ya nguvu za ujana zimepotea sana kwenye
makaburi. Utaniuliza ni kwa nini? Na mimi pia napenda nikuulize je, ulishaweza
kwenda kwa mganga, ulishawashi kutambika, ulishamsindikiza rafiki au jamaa yako
kwenda kutoa mimba, ulishirikia sadaka za mizimu, ulifanya maagano ya
ushirikiana wa aina yeyote ile au mila na desturi ambazo umerithi kutoka kwa
wazee wako?
Tuangalie hivi vichache, tuanze kuangalia kuhusu maagano. Je,
ulishawahi kufanya maagano yeyote, ukiwa ni wewe kama wewe au na ndugu, jamaa,
rafiki, Mungu na hata shetani?
Je, ulishawahi kwenda makaburini kufanya dawa, ulitumwa na
mganga, ulichanjwa chale makaburini, ulienda kumsindikiza rafiki yako.
Tuone 2 Wafalme 1-17
lakini hapa tuangalie zaidi 2 Wafalme
17-18 inasema; wakawapitisha watoto wao, waume na wake, motoni, wakapiga
ramli, wakafanya uchawi, wakajiuza nafsi zao wapate kufanya yaliyo maovu
machoni pa Bwana, hata kumkasirisha. Kwa hiyo akawaghadhibikia Israeli sana,
akawahamisha mbali na uso wake, wala hapana aliyesalia ila kabila ya Yuda peke
yake.
Je, wazazi wako walishawahi kukupeleka kwa waganga, au mimba
yako ulipatikana kwa mganga? Na wakati ulipozaliwa walienda kwa mganga, mila,
matambiko, mizimu kwenda kukukabidhi wa wakuu wa pale?
Pia, walifanya machukizo hayo ambayo kwenye 2 Wafalme 17-18 Mungu anachukizwa nayo
walienda kukufanyia wakiti ukiwa mdogo? Na kama hivyo vyote ulishawahi
kupitishwa huko, tunaona kuwa ndio vyanzo ya kuliwa kwa ujana wako.
Katika Isaya 47:1-15
inasema; simama sasa na uganga wako, na wingi wa uchawi wako, uliojitaambisha
na tangu ujana wako; labda utaweza kupata faida, labda utaweza kushinda.
Umechoka kwa wingi wa mashauri yako; basi, na wasimame hao wajuao falaki,
wazitazamao nyota, watabirio kila mwezi mambo ya mwezi huo, wakakuokoe na mambo
yatakayokupata.
Kuhusu mizimu wengi wetu tumejikuta kumeingia kwenye mtego wa
shetani kwa kushiriki kuabudu mizimu kwa kutokujua au kwa kujua. Ikiwa ni
pamoja na kushiriki ana kwa ana, kuchangia kwa hali yeyote ila ikiwa ni pamoja
na fedha taslimu, vifaa vyovyote vilivyokuwa vikitumika katika kufanyia sadaka
hiyo.
Mila nazo zimetufunga kutokana na kurithi kuto kwa wazee wetu
yaani bila mtu kufanyiwa mila maisha yako hayawezi kwenda ndivyo tulivyokuwa
tukiamini, na unaweza ukasongwa na nuksi, balaa na mikosi haya yote ndio
inayoweza kwa namna moja au nyingine kuharibu nguvu ya ujana wako.
Hapa tunaona kuwa tunaonywa kwa tegemea nguvu za ibilisi
badala ya kumtegemea Mungu anayekupa uhai. Je, tangu uivyotumia uchawi, uganga,
matambiko, mila, ibada za sanamu una nafuu yeyote katika hayo matatizo yanayo
kukabili? Au unasema afadhali ya jana kuliko leo.
Utawezaje kurejesha nguvu ya ujana wako uliopotea.
Unachotakiwa kufanya ni kufanya toba ya kweli yaani ni kumaanisha kuwa unaikana
nafsi yako ya kumwachia Mungu atende.
Kuhusu hadithi ya mwana mpotevua ambaye alidai mali kwa baba
yake na alipopewa alienda kutapanya mali hiyo na makahaba Luka 15: 11-32. Lakini alipoona kuna maisha ya kule ni magumu siku
hadi siku alisema moyoni, ni watumishi wangapi wa baba yangu wanakula na kusasa
nami nataabika hapa.
Akakata shauri ya kurejea nyumbani kwa baba yake na baba
alipomuona alifurahi hakukasirika maana mwanae aliepotea amerudi alimvika vazi,
pete na viatu. Sasa hata wewe umrudia
Muumba wako leo hii ili upate kuvika vazi, pete na viatu.
Unatakiwa pia kufufua nguvu ya maombi ambayo hata kama
hujawahi kufanya, lakini kuna roho ambaye wakati wote yeye yupo ukimtumia
ipasavyo anauwezo wa kukufundisha maombi.
Pia tunatakiwa kujisahehe wenyewe. Imezoeleka mara nyingi
kuwa lazima tuwasamehe wenzetu waliotukosea lakini tunajisahau sisi wewenye
kujisamehe, na kama usipojisamehe wewe mwenyewe nani atakaye kusameme ikiwa
imejikosea wewe mwenyewe?
Hapo ndipo utaweza kurejeza ujana wako uliopotea kwa toba,
rehema, na msamaha. Hujachelewa anza sasa maana leo ni ya kwako kesho hujui ni
ya nini?
Imani, utii,
Roho Mtakatifu.
Chanzo cha
imani ni kusikia. Unatakiwa uwe makini kusikia ndipo utende uliolisikia. Na
ikiwa kama husikii vizuri na ukatenda hicho ulichokisikia ambacho si sahihi
kinaweza kukusababishia matatizo ambayo yataweza kukugharimu maisha yako yote.
Chanzo cha
utii ni upendo bila upendo utii hauna nafasi katika maisha ya mwanadamu. Mungu
alimuumba mwanadamu ili amtii, kwa sababu Mungu wetu ni mwenye wivu kwa sababu
ya upendo alionao kwetu sisi wanadamu. Adamu alivyokula tunda la mti wa katikati ndani ya bustani ile, lakini kwa muda mchache
tu alipoteza ule utii waliokuwa nao kwa kufanya kile ambacho waliambiwa
wasikifanye. Mwanzo 3:1
Upendo wa
Mungu ulionao kwetu sisi wanadamu ni mkubwa ambao hakuna mtu yeyete atakayeza
kuufanya katika ulimwengu huu tulionao hivi sasa. Yeye alimtoa mwana wake wa
pekee ili afe msalabali kwa ajili ya dhambi zetu. Je wewe unaweza kuutoa uhai
wako kwa ajili ya ndugu yako?
Mungu ndiye
aliyetoa maagizo elekezi kwa mwanadamu ya utii kwa maneno yale ya kutokula tunda
lile la mti wa katikati. Walipokosa utii
kwa kumsikiliza shetani walivunja upendo na Mungu pale pale.
Ukitaka kuwa
mtii ni lazima ufanye kile ambacho umeagizwa na kiongozi au mkubwa wako yeyote.
Iwapo ukifanya kinyume cha hivyo ujue kuwa umeshatenda dhambi ya kukusudia au
yakuto kukusudia. Na bila kufanya toba ya aina yeyote ila unakuja mbele za
Bwana na shida zako ulizonazo kuanza kulalamika kuwa mbona hakujibu maombi
yako. Wakati umeshasahau kuwa umemkosea hapo awali. Huko ni kumekosa utii mbele
zake ukaenenda na njia zako.
Ni kitu Mungu
amekitengeneza ili tukiri ile imani ya kumtumikia, utii ndio huonyesha na kukomaza imani yako. Kwa
mfano mtoto nyumbani anapokuwa mtii hupata ziada zaidi ya mwengine. Utii ni
kitu cha lazima katika maisha ya mwanadamu.
Utii ni
fimbo, ni upanga ukatao kuwili. Iwapo ukimuheshimu na kumtii mzazi wako yeyote
atakupa kile utakacho, si kwa sababu u mzuri kuliko wengine bali ni kwa utii
ulionao na unyenyekevu unaomfanyia kutoka moyoni mwako.
Lazima utii
mamlaka tulionao. Kiongozi anapoagiza lazima kila mtu afuate agizo analotoa.
Unatakiwa kuchagua kumtumikia Mungu au kumtumikia mwanadamu. Kazi ya bwana
inatakiwa ipewe kipaumbele ndipo zile nyingine zifuate. Hivyo vyote vitafanyika iwapo kuna utii ndani
yake.
Utii una
kanuni yake kubali kupokea ushauri, kubali kufundishika, kukemewa, kushutumiwa
na hata kutukanwa, wazazi, majirani. Unapopokea ushauri unatakiwa uwe na moyo
wa unyenyekevu. Unapaswa kutenda uliyoagizwa na si kwa mapenzi yako wewe.
Kubali
kufundishika. Kizazi hiki kinapenda kulaumu watoto wao mwa matendo yao maofu
wanayofanya. Wewe kama mzazi au mlezi umekaa na mtoto wako ukamfundisha kuwa,
dunia ya sasa tunatakiwa tuenende hivi na sio hivi. Au tunamwachia mwalimu
ndiye amfundishe? Au umemuacha ajifunze yeye mwenyewe. Jamii ya sasa hivi ina
ukaidi wa kutaka kufundisha vitu hujiona kuwa kila kitu mtu anakijua, kumbe tu
vipofu mbele za Mungu.
Ulimwengu wa
sasa watu wengu hudhulumiwa haki zao kwa kutokana na unyonge waliokuwa nao.
Ikiwa inaona hapa haki yangu imedhulumiwa na kila njia ya haki umetumia bila
mafanikio yoyote yale. Usikate tamaa njoo mbele za Bwana umlilie, kumbuka Mungu
wetu ni mkuu kuliko huyo anayekudhulumu haki zako. Muhubiri 5:8
Waebrania 12:5-8 ukikemewa naye kupitia matendo yako
ukikaidi kutokana na kiburi chako hapo utakuwa hauna utii. Viongozi wawe wakali
katika kanisa katika kukemea mambo yasiyompendeza Mungu. Baadhi yao wanaogopa
wakiwakemea waamini wao wanaweza wakaogope. Je, hapo utakuwa unamtii Mungu au
unatii mamlaka ya mwanadamu?
Utii ni
silaha ya vita zote duniani. Mwanadamu hapo ulipo uko kwenye vita kila dakika. Kumbuka
kuwa Mungu hupitia kwa mwanadamu na shetani pia hupiti kwa mwanadamu. Ni utii
peke yake ndio utakaokusaidia kushinda vita hizo.
Vita hizo ni
kati ya mwanamke wa shetani uwanja wa vita ni bustani ya Edeni. Edeni ni kila
mahali ulipo wewe mwanadamu. Hii ni vita pekee ndio shetani aliyoishinda hapa
duniani. Vita hiyo ilizidi kuwa ngumu pale Mungu alipoweka uadui katika ya
Mwanadamu ya Mungu. Mungu alivyoona shetani amezidi lakini Mungu alileta uadui
kati ya nyoka na mwanadamu. Ndipo shetani alishindwa kwa Yesu kufa pale
msalabani kwa ajili ya dhambi walizotenda wanadamu.
Mama apatapo
mimba humchukia mumewe kwa sababu kuna mwanya ambao shetani ameingia ndani
hapo. Mtoto huchukua tabia zile za kale ambazo sheetani aliwahi pindi mtoto
alipotungwa mimba.
Shetani hufuatilia mimba ya mwanamke tangu
siku ile apatapo mimba. Ndipo watoto wengi wazaliwapo huwa na tabia tofauti kwa
sababu ya shetani kuingilia ujauzito ule. Na watoto kuwa na tabia tofauti
katika nyumba moja. Tumekombolewa kwa
utii wa yesu pale msalabani kwa kuangikwa kwake.
Vita
nyingine ni uasi na utii uwanja wa vita ni Kaini na Abeli. Iliacha kudaiwa
baada ya Yesu kuangikwa pake msalabani. Kwa damu ya Yesu kumwagika pale Kalvari.
Vita nyingine
ni ya uovu na wema. Uwanja wa vita ni duniani. Sodoma na Gomora. Ndoa za jinsia
moja baadhi ya nchi huidhinisha kwenye katiba zao. Unatakiwa kujiepusha na hayo
yote kwa kuwa utii mbele za Bwana tu.
Macho yako
huangalia nini? Wengi wetu hupenda kuandalia vitu ambavyo ukisha fanya mazoea
ya kuangalia vitu hivyo unaweza ikakusababishia kuuondoa uwepo wa Mungu katika
macho yako na hivyo ukachafua hekalu la Mungu ambalo ni mwili wako kwa
kuangalia kwa macho, kisha ukapatwa na tamaa ya mwili ukaangukia dhambini. Kataa
mchezo wa kunajisi macho yako. Omba rehema kwa dhambi ambazo huzijui.
Kuna watu
walishatolewa pepo kutokana na kuangalia luninga. Na ikiwa huamini hivyo kuwa
shetani anaweza akamuingia mtu kutoka kwenye luninga anayoiangalia. Iwapo mtumishi akasema kuwa weka mkono kwenye radio
na ukapona. Je, wewe unayeangalia luninga usishangae vitu vya shetani
vitakupata wewe moja kwa moja. Je, utamsingizia nani aliyekufanyia hivyo. Je
si, wewe uliyejitakia yote hayo kwa tamaa zako za mwili.
Watu wengi
huogopa kuwakosoa watu walio karibu nao kwa kuogopa kuchukiwa iwapo atamwambia
ukweli. Usikasirike kumkosoa mwenzio hata kama atakuchukia ni heri uiokoe roho
yake kuliko kuiacha iangamie.
Kwa kila
jambo tufanyalo hapa duniani tunatakiwa tumshukuru Mungu kwa yote. Tukumbuke
tunapomshukuru Mungu kwa kila jambo, ili imani yetu ihubiriwe ulimwenguni kote.
Warumi 1:8
Vita ya Imani
potofu imani na imani ya kweli, uwanja wa vita Red Sea. Vita hivyo ilipiganwa
kati ya Mungu na Shetani kupitia wana wa Israeli,ndipo Farao na jeshi lake
waliishia Red Sea (Bahari nyekundu). Wewe pia una Bahari nyekundu katika maisha
yote ya kila siku, je uwatezaje kuvuka katika bahari hiyo ni kwa kuwa mtii kusikia, mnyenyekevu na upendo.
Vita
nyingine ni kati ya Kiza na wana wa Mungu,
uwanja wa vita inapopiganwa ni Duniani. Jinsi ya kushinda vita hiyo ni kuwa
mtii kwa kuliitia jina la Yesu kila iitwapo leo.
Vita
nyhingine ni kati ya Manabii wa kweli na
uongo. Utajuaje kuwa huyu ni nabii wa ukweli na huyu ni nabii wa uongo. Kwa
kumtumia Roho Mtakatifu utaweza kusikia sauti ya ambayo itakuonyesha kuwa nabii
huyu ni nabii wa kweli. Elia alishinda hiyo vita kwa uwanja wa Kalmeli. Nabii wa
kweli huwa hana watu wengi, tukumbuke kuwa
njia ile ni nyembamba iendayo uzimani. Watu wengi hufuata manaabii wa
uongo kwa kukosa maarifa ya Kiungu. Tumia macho, masiko
Vita ni kati
ya Mikaeli na Lusifa vita hii inapiganwa kati ya Jeshi la Bwana na Jeshi la
Uovu. Isaya 14:12:15. Katika vita
inayokukabili katika maisha yako usipigane mwewe mwenyewe mtumie Malaika Mikaeli
akupe upanga wake ili upigane vita hivyo.
Vita nyingine
ni kati ya toba na dhambi, uwanja unaopiganwa vita hivyo ni duniani. Watu
hawataki kutubu dhambi zao. Tena hujifanya hawazijui kwa makasudi kwa kuogopa
kuzitamka mbele ya makuhani. Kwa kukosa
utii shetani hukufunika kwa kutokusema hizo dhambi zako. Kwa nini unaogopa
kusitamka dhambi hizo, mbona kuna mitume ambao walifanya dhambi hapo awali
lakini walipo tubu tu walikuwa huru na sasa wanaitwa watakatifu huko mbinguni?
Vita
nyingine ni kati ya Nuru na Giza. Bustani ya Edeni, vita hivyo vilipiganiwa jagwani
Mungu ndiye aliyeingilia kati. Jangwani alitoa nguzo ya moto ili kuongoza wana
wa Israeli ni alama ya kuwaongoza. Kinyume cha utii watu waliiba vinyago vya
waisraeli wakashindwa walipovichoma moto walishinda vita hivyo.
Watu wengu
hutaka vitu vya gizani kuliko vya nuru. Iwapo utakuwa na subira mbele za Mungu
atakupa vitu ambavyo shetani alivificha gizani, yeye Mungu atakupa vyote vya
gizani.
Vita
nyingieni ni ya Mwili na Roho, vita hivyo hupiganwa mwilini. Wagalatia 5:17 usiendekeza mwili wako kwa
uchafu wa aina yeyote ile hilo ni hekalu la Bwana. Kumbuka unapochafua mwili
wako unamfukuza Roho Mtakatifu awe mbali nawe kwa hivyo utabaki wewe peke yako
kama kopo tupu. Majambazi wanaiba na kuua ni vita ya mwili na roho. Mume na mke
kwa sababu ya mali ni vita vya mwili na roho.
Ipe nafasi
roho itawale. Achana na habari ya mwili. Iwapo utafanikiwa kushinda utapata
hitimisho ya roho yako.
Vita
nyingine ni kati ya Mali na Mungu. Mungu
alitupa hapa duniani kumiliki, watu wangi huabudu mali kuliko Mungu. Viongozi
wengi wa dini wanakusanya mali kutoka kwa waamini na kuua nguvu za waamini
kushiriki kikamilifu katika kumtumikia muumba wao.
Fedha na
dhahabu ni mali yake. Wewe unayeifanya kuwa ni yako umeitoa wapi. Ikiwa yeye
anakupa kisha wewe hutaki kumtolea, ndio maana leo una mali nyingi lakini kesho
huna kwa sababu hukuacha wewe kwa kuto kumrudishia kile alichokupa ukakipoteza
kwa njia za uovu, yeye huenda kuwapa watu wake wanaomtii na kumheshimu.
Mahali pa
juu na chini uwanja wa vita ni kichwani kwako. Elimu ya Mungu Efeso
6:10. Tumia elimu ya mungu kuondoa elimu upotoshayo, udanganyayo,
Watu wa Mungu
giza uwanja wa giza mwenyewe. Ili maisha yako yaweze kuwa mazuri unatakiwa
ushinde vita ya upendo. Mahali penye upendo pana amani, haki, utulivu,
uzalishaji wa kutosha, utele wa chakula, nyumba, magari chanzo cha yote ni
upendo. Na kama huna upendo ni bure kabisa. Huwezi kumpenda mtu kama hauna
utii. Utii
Vita
nyingine ni Ubongo na elimu ya Mungu, uwanja uaopiganiwa vita hivyo ni masuala
ya ibada hupiganwa na pale unapopungukiwa na hekima huwa na kujionyesha
(showoff). Ubongo wake hupambana na ubongo wa Mungu.
Ukiwa na
utii huwa na imani ya Mungu ambayo hutengeneza nguvu ya kumshinda ibilisi. Utii
huanzia kwako mwenyewe. Hujitii kiasi gani unavaaje, unatembeaje, unasemaje,
mahusiano mbele za watu.
Nyumba ya
bwana ni mahali patakatifu. Musa aliambiwa vua viatu mahali hapa ni patatifu.
Iweni safi mwilini na rohoni.
KWA NINI
TUNATEMBEA KATIKA MATESO
Tujiulize
mimi na wewe kwanin kwa nini tunatembea katika mateso. Ni kwa sababu ya makosa
yetu, makosa waliofanya wazazi wetu, makosa waliofanya ndugu wa familia moja
niliozaliwa nao,jamaa zangu wanaonizunguka au ya ukoo ninaotoka.
Na ukisha jichunguza kote huko unatakiwa
utafakari ni kwa sababu ya kumemwacha
Mungu na kutegemea nguvu zetu wenyewe ana tuna miungu mingine ambayo tunaiabudu.i
Hii yote
inatoka na kujiona kuwa Mungu huyu tuliyemzoea naweza nikamuomba kitu fulani
leo, kesho akanipa tu, lakini nikisha ona kila siku ninapomuomba Mungu anatenda
basi hujifanyia kuwa ni mazoea. Lakini tuelewe ya kuwa Mungu wetu hazoeleki
hata kidogo, ni mpya kila iitwapo leo.
Yeremia 4:22 Wapumbavu, waliopungukiwa na akili. Mungu
wetu hana iyana ametupa maarifa tele lakini kwa maarifa tulionayo tuna viburi
vya kwa kumjaribu Mungu. Mwanadamu hataki akutane na majaribu yeyote yale huta
njia ya mteremko tu na pindi apatapo majaribu huanza kuhoji mbona napitishwa
kwenye majaribu yote haya, na kuhoji kuwa je, Mungu wewe upo.
Watu wengi
hujiuliza pia kwanini napitishwa kwenye majaribu hote haya wakati wale wa
shetani wapatwi na mateso au majaribu makubwa. Lakini kaa ukijua kubwa
umeshasema watu wa shetani pale hawapatwi na majaribu kwa sababu pale kwa
shetani ndipo wako nyumbani kwao. Nikuulize wewe uko nyumbani itawezekanaje
mgeni aje akufanyie fujo nyumbani kwako, hivyo ndivyo walivyo watu walioko kwa
shetani ni wako nyumbani kwao.
Majaribu yanaweza kutupata kutokana na kutojua
au kukaidi sheria za Mungu. Hivi vyote tunatakiwa ujitafakiari kuwa wewe
unazifuata sheria hizo au unaendelea kufuata utaratibu au sheria yako uliouzoea
tangu hapo awali?
Kumbukumbu Torati 11:13 ikiwa wewe ni mtoto pindi mzazi wako
akakuonya kwa matenda yako ambayo hayampendezi lakini wewe ukaendelea kukaidi
yale maonyo unayopewa na wazazi wako. Mwisho wa yote mzazi huchoka kwa ukaidi
wako hivyo huacha ulimwengu ukufunze hapo pia unawafukuza wake malaika walizi
wanaokulinda ili usianguke, matokeo yake unabaki kopo tupu. Tukumbuke kuna
methali isemayo‘asiyefuzwa na wazazi hufunzwa na ulimwengu’.
Kumbuka kuwa
ukienda kinyume na mapenzi ya Mungu naye atakuacha, ndipo hapo shetani hupata
nafasi ya kukumiliki kuanzia rohoni hadi mwilini. Maana shetani huanza
kukuharibu rohoni hapo ukishaharibika matokeo ya kuharibika kwako huonekana
mwilini ambapo yeye ameshamaliza kazi zake zote hufurahia ushindi huo kwa
kukufanya kuwa fungu lake.
Kuna baadhi
ya wanadamu akisifuwa tu kuwa yeye ni mzuri idara zote basi hapo huanza
majivuno, jeuri, uzinzi wa kujionyesha kuwa yeye ni tofauti na wengine kumbe katika Yeremia 4:31 anatuonya kwa kuto
kudanganyika na sifa ambazo wanadamu wenzetu nazotupa. Kwani sifa hizo wengine
wanatoa sifa kwa sababu ya maslahi yao binafsi. Uwe makini kwa kila akupaye sifa kwani wengine
ni wakala wa shetani hutafuta mbinu za
kukuangusha.
Kila iitwapo
leo unaenda mbele za bwana kuungama dhambi zako au unajihesabia haki muda wote,
njia zako ni nyingi unawaendea wageni ambao ni miungu ambayo iliyoko chini ya
miti mikubwa, majabali, mapango, baharini, njia panda, kwenye mito na hata
vijito huko kote huko ulienda kupata ya ziada kuliko Mungu anayokupa. Yeremia 2:13 Uovu huu wa kumwacha
Mungu, unasababisha mabirika yetu kuvuja.
Inawezekana
kuwa kuna mahali hatupo sawa kimawazo, kimaneno na kivitendo na Mungu, ihali
tunadai kupokea kutoka kwake. Wakati mwingine tunaenda mbele za Mungu huku
mabirika yetu yanavuja kwa kujua au kutokujua, hii yote ni kutokana na mioyo
yetu na roho zetu ziko mbali na Mungu. Hofu ya Mungu hatunayo tena tunaenenda
kwa akili zetu tu bila kujua kuwa tunakoonda tunaenda kutumbukia shimoni.
Pindi
unapovushwa kwenye majaribu ukapita salama kumbuka kuwa Mungu alikuwa nawe
wakati wote huo. Hivyo usisahau kumpa Mungu shukrani kwa yote anayokutendea na
hapa yule ambaye hajawaji kupitishwa
katika majaribu vivyo hivyo unatakiwa
uje mbele za Bwana kwa shukurani kwa sadaka, zaka na dhabihu ili mpate
kuinuliwa zaidi ya hapo pia usisahau kumtolea Mungu nadhiri zako zote kwa maana
unapojiungamanisha na Mungu ndipo mahali pako salama unapojichagulia katika
ulimwengu huu. Kumbukumbu la Torati 12:11
Umejilindaje
na choyo, hapo Luka Mtakatifu anataka
ujitafakari wewe kama wewe katika ulimwengu huu uliojaa anasa na machukizo
mbele za Mungu. Luka 12:15 anasema,
Tujilinde na choyo maana uzima wa mtu
haumo katika wingi wa vitu vyake alivyonavyo. Tutafute heri kwa kumtolea
Mungu
Wakorinto 2: 4-16 Utu wa nje unachokaa lakini utu wa
ndani unatakiwa uwe na nguvu pia uwe imara na hata kama utakuwa unajaribiwa
katika mapito yeyote yale unayopitia. Usije ukaucha utu wako wa ndani uharibike
kwani unapoharibika utu wako wa ndani kwa dhiki hiyo ya nje, kumbuka
usiviangalie vinavyoonekana kwani hivyo ambavyo ninaharibu utu wako wa nje,
bali viangalie sana tena kwa macho mawili vile ambavyo havionekani ambavyo ni
vya milele.
Maisha yako
ya utaishije hapa duniani umejiuliza wewe mwenyewe au umemshirikisha Muumba
wako. Je kwa akili zako unaweza kuishi hapa duniani bila maada wowote utokao
kwa Mungu?
Lakini Isaya 45:11 anakujibu swali hilo na
kusema, Bwana Mtakatifu wa Israeli Muumba wake, asema hivi; Niulize habari za
mambo yatakayokuja; mambo ya wana wangu, na habari za kazi ya mikono yangu;
haya! Niaagizeni. Je, umemuuliza vingapi katika maisha yako, watoto, ndugu,
jamaa na marafiki wanakuzunguka? Na kama ulisha muuliza je umemuagiza akufanyie
nini hapa duniani?
Kumbuka kuwa
kama kila ufanyalo haliendi na kila utendalo halifanikiwi unapaswa umshirikishe
Muumba wako ndiye yeye ajuaye yote yajayo na yakupatayo kwenye maisha yako na
familia yako, kazini, kwenye biashara zako na hata kwenye kazi zozote zile
ambazo si kinyume na yeye na umuagize unataka nini akufanyie. Kumbuka kuwa si
kwa mapenzi yetu bali kwa mapenzi yake yatimizwe.
KUKOMBOA UZAO
KUMTUMIKIA MUNGU
Katika
maisha ya kila mwanadamu lazima kila mtu amezaliwa na wazazi wote wawili. Asiye
zaliwa na wazazi wote wawili nia Adamu na Eva tu. Lakini kizazi kilichofuatia
baada ya hapo wote wana wazazi wawili.
Kuna aina
nyingi za uzao, lakini leo tuangalie uzao wa damu. 1 Petro:1:23, anasema kuwa tumezaliwa mara ya pili, si kwa mbegu
inayoharibika. Lakini mtoto anapozaliwa kumbuka kuwa shetani huko mlangoni
akisubiri akitafuta kile ambacho mtoto anapozaliwa na kitu chake cha Kiungu
akiharibu wakati ule ule.
Mtoto hana
tofauti na mtumwa Wagalatia 4:1.
Mtoto anapozaliwa huwa mzazi au mlezi wake ndiye anayekuwa kiongozi wake kwa
kila kitu hadi hao atakapokuwa na fahamu zake za kuweza kujitegemea mwenyewe.
Mwivi haji
ila kuiba na kuharibu na hata kuchinja Yohana
10:10, kumbuka kuwa mwizi yeyote anayeenda kuiba haendi pale kwa kutoa
taarifa kuwa anakuja kuiba, wewe hushitukia tu kuwa ameshakuja kuiba. Sasa
shetani ndiye mwivi wetu wa vile ambavyo Mungu ametupa sisi tangu kabla
hatujaumbwa na hata tukiwa tumboni mwa mama zetu na maisha yetu yote.
Mtoto yeyote
anajifunza kutokana na kujifunza, kuona na hata kusikia kutokana na wazazi wake
wote wawili. Pindi mtoto anapokuwa tumboni na baba na mama wakawa na ugomvi
yule mtoto ulieko kule tumboni naye hushiriki kwa namna moja au nyingine ugomvi
ule kwa njia ya kusikia.
Watu wengi
husema kuwa mama akiwa mjamzito ni chanzo cha magomvi kati ya baba na mama. La
hasha hii inatokana tu na wewe kutokumshirikisha Muumba wako tangu siku ile ya
kwanza ulipopata ujauzito huko. Kumbuka pindi upatapo ujauzito mshirikishe
Muumba wako kwa kila kitu maana mwili huo si wako peke yako ni wa Mungu pia.
Usipo
mshirikisha Mungu tangu kipindi chako cha kwanza upatapo ujauzito wako kumbuka
kuna mharibifu ambaye anasubiri wewe ulime shamba hilo yeye anasubiri unapoenda
kulala apande magugu. Je, wewe kuna ambaye amepanda magugu kwenye uzao wako?
Pindi mtoto
anapozaliwa na kukua, kasha ghafla akabadilka tabia yake, msije mkafarakana
baba na mama kwa ajili ya mtoto huyo rudini nyuma huku mkitafakari kuwa je ni
wapi tulipokosea tukamrudia Mungu. Je, ujauzito ulipotokea tuliukabidhi mbele
za Bwana au tuliona hapa tulitengeneza sisi wenyewe? Fungua mafundo hayo ambayo
yamempata mtoto mpaka anakuwa na tabia ambazo hakuna hata mzazi hata mzazi
mmoja wenu aliyekuwa nazo.
Uzao wa
tumbo lako ni thawabu Zaburi 127:3.
Usilaumu uzao wako hata siku moja. Wewe kama mzazi unatakiwa usimame kwenye
nafasi yako kama mzazi. Nguvu uliyonayo inamfuata mtoto popote pale alipo kwa
wewe kusimama na Bwana. Tumia mamlaka uliyonayo kama mzazi ambaye ni Mungu wa
hapa duniani.
Mtoto ni
mbegu ambayo hupandwa kwenye tumbo la mama na kisha hupatikana kuwa ni mche
anapozaliwa. Na akisha kuwa mtoto huyo hutoa matunda ambayo katika familia
huleta furaha na upendo katika familia.
Kuna vitu
vinavyoharibu uzao. Moja ya vitu hivyo ni maagano. Naomba nikuulize wewe mzazi
ulishawahi kufanya maagano yeyote yake kabla ya kumpata huyo mtoto na baada ya
kumpata huyo mtoto umetimiza hayo maagano?
Kuna maagano
mengine ni mazuri na maagano mengine ni mabaya, kati ya haya mawili wewe
ulifunga agano lipi, baya au zuri. Na kama lifanya maagano ya kumtolea Mungu
kila upatapo kumbuka kumrithisha mtoto wako maagano hayo. Mfano, mzazi anaweza
kuwa ni mtoaji mzuri sana na akabarikiwa kupata mali nyingi. Lakini akifa mali
zote zikaenda nae. Hapo anakuwa hajawarithisha watoto wake lile agano
alilolifanya na Mungu.
Angano
linguine ni lile baya. Maagano haya utokana na mzazi kutafuta mtoto kwa njia
isiyompendeza Mungu. Inawezekana mtoto uliyenaye umempaka kwa njia za wagaga na
matambiko au hata njia nyingine unazozijua wewe.
Ukaambiwa
kuwa ukitaka kupata ujauzito lazima uzini juu ya kaburi, au unapooja kaburi
limechimbwa wewe nenda kachukue mzizi kule ndani ya kaburi, kwa tamaa yako ya
kupata mtoto ili ndoa yako isiharibike ukafanya masharti yote hayo uliyopewa na
mganga. Ukenda ukafanyiwa dawa ukapata ujauzito.
Kumbuka kuwa
mzizi wowote una nguvu na kaburi nalo lina nguvu hapo utakuwa umemrithisha
mtoto maagano ya kuzimu. Na hata maisha yake yote yatakuwa ni ya mateso matupu.
Kumbuka shetani ni muharibifu wakati wote.
Ni nani
awezae kutoa kitu kisafi kitoke kwenye kwenye kitu kichafu ni Mungu peke yake.
Yeye huweza kumtoa mtu aliyepotea katika uchawi, ulevi, wizi, uasherati na vitu
vingine vingi.
Usije ukafa
na deni kabla ya Yesu kurudi tena mara ya pili. Kumbuka kufufua zile huduma
ambazo zimekufa kwenye nafsi yako kwa kumshirikisha Roho Mtakatifu.
Watu
wanaweza kupatwa na madhara ya kupighwa kutokana na mzazi kuchukiana na mtoto. Malaki 4:5,6 inatuonya kuwa ugomvi kati
ya baba na mtoto ataipiga dunia kwa laana. Umuonapo jirani yako wana ugomvi na
mtoto wake kuwa moja wao wa kusuluhisha ugomvi huo kama ikishindikana wewe
ingia magotini umwambie Mungu aingilie kati ugomvi wao huo.
Wazazi
wasiwe vyanzo vya kuwatawanya watoto wao , hata kama mzazi mmoja wapo ana mtoto
nje ya ndoa ni heri ukamharifu mwenzako kuwa una mtoto nje kuliko kungojea siku
unataka kukata roho ndipo unamwambia. Hivyo utakuwa unajitesa wewe mwenyewe na
utaondoka na mzigo wako.
Mungu alimuumba mwanadamu kwa thamani kubwa sana, alimpa akli
yenye ugunduzi ndani yake. Mwanadamu ameumbwa kwa mfano wa Mungu mwenyewe,
lakini shetani yeye ni kiumbe kama malaika wengine.
Maisha anayoishi shetani ni ya sehemu moja nayo ni kuzimu. Na
akitaka kumdhuru mwanadamu yeyete humtumia mwanadamu kumuharibu au kumdhuru
mwanadamu mwenzie. Yeye shetani hana uwezo wa kumwingia mtu moja kwa moja.
Unachotakiwa kufanya ili kumuepuka huyo shetani, wewe
mwanadamu ili shetani asipata mlango wa kukuingia unatakiwa uishi katika
viwango vya uungu.
Bwana amekuweka kwenye bustani yake hapa dunia ili uweze
kuilima na kuitunza. Mwanzo 2:15
ikiwe wewe umepewa bustani ulilime na uitunze je, hadi hivi sasa umeilima hiyo
bustani na Mungu na kuitunza mazao yake. Kama umeilima je unakesha kuituza.
Maana shetani yuko wakati wote akizunguka zunguka ili apande magugu ndani yake.
Kumbuka kuwa macho wakati wote ukikesha kwa kuomba.
Kumbuka neno lako ni sheria malangoni pa adui. Usimuwekee
Mungu mashaka unachotakiwa kufanya ni kutii na kumuamini. Wengi wa watu
wanamuwekea Mungu mashaka ikiwa maombi yao yanachelewa kujibiwa kwa wakati ule
aliyoomba.
Mungu wetu si kigeugeu humpa mtu kile anachostahili na si
atakacho yeye mwanadamu. Na humpa kwa muda na wakati ufaao. Unaweza ukaomba uwe
tajiri lakini Mungu akakupa kwanza elimu. Hiyo elimu ukiitumia vizuri ndipo
kitakuwa chanzo chao cha utajiri.
Unachotakiwa kuzingatia ni Yohana 12:24, chembe ya ngano
isipoanguka ikafa haitoi mazao. Vivyo hivyo mtu asipokufa katika Mungu hawezi
kuwa mtumishi wa Mungu. Kubali kufa ili mbegu itakayozaliwa kwako iwe mbegu
zuri na ya mfano mbele za watu.
Mungu ametutupa katika nchi sisi kama mbegu ili atuinue upya
katika yeye. Ufanyapo kazi yoyote kwa elimu uliyokuwa nayo kwa upendo wa Mungu
hakika, Mungu huyo huyo atakuinua. Bali ufanyapo kazi kwa matakwa yako wewe
mwenyewe hakika hutafika mbali na mwisho wa yote utakuwa ni majuto, maana hapo
umempa nafasi shetani afanye kazi na wewe bila ya wewe kugundua kuwa umempa
nafasi hiyo shetani.
Unapoambia kwenye ulimwengu wa roho kitu fulani umpe mtu
fulani, basi usifanye mashaka ya kutoa kitu hicho ulicho nacho kumpatia mtu
uliyeambia na hata kama kitu hicho ndio umetoka kukinunua dukani au umeletewa
zawadi. Pia elimu uliyokuwa nayo usiwe mchoyo kwa kuwasaidia wengine kwani
ufanyapo hivyo utakuwa unamtangaza Mungu kwa elimu uliyo kuwa nayo.
Ili uwe na amini moyoni mwako unatakiwa utumike na Mungu.
Wekeza katika Mungu hapo hakuna hata yule kibaka, shetani, mzimu, majini,
vibwengo, vinyamkera, mchawi, ambaye
anaweza kuiba ambavyo umeviwekeza kwa Mungu.
Chochote unachokipanda kwa ajili ya Mungu hutangulia
kukuandalia mazingira. Kati ya Mungu na shetani wewe unamtumikia nani? Matendo ya Mitume 19:13 mtu alikuwa
anatolewa pepo, lakini wakati akitolewa yule pepo akamwambia yule mtoa pepo
kuwa Yesu wanamjua na Paulo wanamjua lakini wewe unayetutoa ni nani? Usije ukamwambia mwenzio mdhambi kumbe wewe ni
mdhambi zaidi yak wake.
Iwapo Samweli alimtumikia Bwana mbele ya Elia. Je wewe
unamtumikia nani mbele ya nani? Au unajitumikia wewe mbele ya nafsi yako na
Mungu umemuweka kando? Lazima umtumikia mtu mbele ya Bwana. 1 Samweli 3:1
Katika utumishi huo huo Joshua alikuwa mtumishi wa Musa. Pia
Elisha alitumika kwa Elia. Hapo utaona manabii wa zamani wakuwa watumishi wa
watu ndipo wakaja kuwa wakuu baadaye. Usipokubali kutumika sasa hutaweza kuwa
mkuu.
Heshima siku zote hauwezi ukaileta wewe kwa elimu, ujuzi,
akili au maarifa uliyokuwa nayo. Heshima siku zote hujitetea yenyewe 1 Samweli 3:21.
Iwapo unataka kuwa mtumishi katika hema ya Bwana lazima
mtafute mtumishi ambaye yuko zaidi rohoni na sio mwilini. Ili aweze kukujenga
kiroho na kiimani zaidi. Tumika mbele ya wachungaji, manabii, wainjilisti ili
upate upako wao nawe uweze kufikia kile kiwango wambacho ulikuwa unatamani uwe
nacho. 2 Nyakati 26:5 aliyemtafuta
Bwana siku ya maono atampata.
Kwa hiyo usikate tamaa kwa njia unazopitia za kumtafuta
Kristo. Wewe ukishindwa ungia magotini umuulize kuwa mimi hapa nakwama nifanye
nini? Usiitegemee nafsi yako kufanya jambo ambalo liko nje ya uwezo wako.
KUFUTA MASHTAKA YA KIZAZI
KUFUTA MASHTAKA YA KIZAZI
Usipotaka usiku huta weza kupata siku ya pili. Usipo kubali
kuwa na usiku katika maisha yako ya kawaida hapa duniani huwezi kupata siku ya
pili. Hapa ina maana unapopatwa na majaribu katika maisha yako lazima kuwe na
mlango wa kutokea.
Kila mfanyabiashara lazima atumie mtaji ili faida ipatikane.
Na asipotumia mtaji hutafahamu katika biashara yako kuwa umepata faida au
hasara. Katika maisha yako lazima unapofanya kazi lazima faida yake ionekane
ndipo ungundue kuwa kazi ninayoifanya ina faida kwangu.
Pindi mtu apatapo matatizo katika maisha yake ya kila siku
lazima utataka kumjua Mungu kilazima, ikiwa wawe ni mtoto wa Mungu. Matatizo katika maisha yanapokuwa
katika kiwango cha juu, hapo ndipo juhudi ya kumtafuta Mungu huongezeka zaidi
ya ile mara ya kwanza ulipoliona tatizo ukadhani kuwa litaisha muda si mrefu.
Kumbe ndio siku inavyoziku kupita ndivyo machungu ya tatizo yanazidi afadhali
na jana.
Majaribu yeyote yanayoletwa na Mungu lazima kuna mlango wa
kutokea, 1 Wakorintho 10:13. Unapopatwa na matatizo
lazima uwe na ustahimilivu, uwe na uwezo wa kuvumilia hiyo tatizo au matatizo
hayo. Usiyumbeyumbe kwani hapo ndipo ukijisahau tu kidogo ndipo unampa shetani
mlango wa kuingilia.
Umeshawahi kujichunguza kuwa wewe ni kizazi gani na kinatoka
wapi? Jitafakari katika maisha yako kuwa wewe u kizazi gani cha nyoka au cha
Mungu. Kizazi chako kiko sahihi au kimeuzwa kutoka na mila na destruri
tuliorithi kutoka kwa wazazi au walezi
wetu.
Kwa karne ya siku hizi za teknolojia kuwa vizazi vingi watu
wameviuza wenyewe kutokana na kutaka maisha rahisi na ya kifahari. Ukitaka
kumfuta Mungu siku zote lazima ukutane na majaribu mengi. Njia ya kumuendea ni
nyembamba huwa na milima na mabonde hakuna tambarare.
Ikiwa umeshawahi kukutana na muwindaji ukamuuliza jinsi
anavyowinda atakueleza kuwa lazima uwe ni mtu jasiri. Maana ukiwa jasirisi hata
ukikutana na mnyama mkali kama samba akikuona wewe u jasiri lazima atakimbia
atajua hapa leo sipati kitu. Lakini ukiwa legelege kwa sekunde tu umeshakuwa
kitoweo chake kizuri.
Mara nyingi shetani hutumia mbinu ya kupandikiza hofu kwa
mwanadamu na hofu hiyo ikisha kuwa na mizizi ndipo udhaifu unapo jengeka. Na
ukisha jengeka huanza kuwa mnyonge. Hii yote shetani hutumia mbinu ya
kupandikiza sumu ya maneno. Maneno
huweza kuleta madhata makubwa katika maisha yeyote ya binadamu.
Mfano mgonjwa anapoenda hospitalini na kukutana na tabibu na
yule tabibu akamuambia kuwa, kwa ugonjwa huu ulionao sikua kama utapona hapo
ametumia maneno kumuambia mtu. Na yale maneno yanapopata nguvu kutoka na
kujirudia rudia akilini hujenga hofu na ile hofu humuongezea mtu ugonjwa ule
mara mbili zaidi hapo ndipo unaweza ukafa haraka kutoka na hofu ulioyokuwa nayo
kutokana na maneno uliyoambiwa na tabibu yule.
Ikiwa katika familia kuwa mtu ana utumishi ndani yake lazima
shetani hutumia mbinu wakati akiwa mdogo kuharibu utumishi wake huwa kabla
haujachipuka mizizi ya utumishi. Humtafuta kizazi kile kikiwa bado kidogo hukizonga
zonga kwa magonjwa hata kila aina ya matatizo ambayo mtu mwenye roho nyepesi
anaweza akaanguka mwenye mikono ya ibilisi kwa kutafuta msaada wa haraka kuliko
kuvumilia kwa kumwomba Mungu.
Naye Kutoka 21:1
anasema, atawapatiliza maovu ya baba zenu kutoka kizazi hadi kizazi. Hapa
kinaongelewa vizazi vinne. Toka babu, baba, mtoto na mjukuu. Kizazi ndio mara
nyingi shetani hukishitaki. Kumbuka Musa alipozaliwa alitaka kuuwawa lakini kwa
neema za Mungu alihifadhiwa kati kati ya maadui. Je, wewe umehifadhiwa katikati
ya maadui zako au hujifahamu kuwa wewe umehifadhiwa katikati ya maadui zako?
Ukiwa unajiona kuwa matatizo yako hayaishi siku hadi siku
umetubu hadi umesahau ulichokuwa unatubu mbele za Mungu. Kumbuka kuwa kizazi
chako ni cha Injili. Umezaa mfalme, nabii, mwinjilisti, shemasi, na vipawa
vingine vingi ambavyo siku zote huwindwa na maadui pande zote ili wakiangamize
kizazi hicho.
Iwapo wazazi wako walitenda dhambi nasi pia tumebeba uovu wao
Maombolezo 5:7. Iwapo baba au mama
yako alishiriki kwa namna mmoja au nyingine kutenda uovu wa aina yeyote ile,
haijalishi alitenda wakati gani iwe kwenye mchana au usiku. Na hata wakati
mwingine mzazi huyo alitenda uovu huo kwa siri, ujue kuwa lazima uovu ule
utakipatiliza kizazi chake, yeye anaweza asione madhara kwa uovu ule alioutenda
lakini anakipa shida kizazi chake kwa kubeba uovu wake.
Kumbuka kuwa kizazi kina malango yake, mbingu yake, nchi
yake,mbawa zake. Pia kina uweza wa kuficha wengine. Kila mbingu ina ardhi yake, kila nchi ina
mazao yake ambayo huvunwa humo. Kila kitu kilichokuwa na mabawa lazima huwa na
uwezo wa kuruka.
Ee mtu wa Mungu lazima uwaambie watu ukweli hata kama
utachukiwa kwa sababu ya ukweli huo. Usikisahau pia kizazi chako kukiambia
ukweli maana unapouhubiri ukweli ndipo uhuru kufunguliwa kutokana na minyororo
ya shetani unapopatikana kwenye maisha ya kizazi chako.
Mara nyingi shetani huishitaki ndoa. Ndoa yeyote hushitakiwa
na shetani kutokana na mmoja kati yao akienda kinyume na mapenzi ya Mungu kwa uzinzi, magomvi, uchawi, na vitu vingine
vingi basi hapo ndipo ummpa shetani kibali cha kukushitaki.
Ndipo hapo mtoto anayezaliwa huambukizwa fangasi hizo za
magomvi, uzinzi, uchawi, matusi na mengine mengi. Mtoto hurithi tabia zote hizo
ambazo wazazi walizomsababishia na humpekelea mtoto kuwa na nembo ya uchungu
moyoni wakati wote.
Tukumbuke Ayubu alikuwa mtu mcha Mungu sana na alibarikiwa
kwa kila kitu ikiwa ni kwa mali, watoto na vitu vingine vingi ambayo ni ndoa,
mifugo, watoto, mali na vitu vingine vingi alibarikiwa navyo. Lakini shetani
kwa hila zake aliona kuwa Ayubu alimcha Mungu kwa sababu amebarikiwa kwa mali
zake. Akamuomba Mungu ruhusa ili amjaribu Ayubu kama kweli anamcha Mungu kwa
kila kitu.
Kumbuka Ayubu alipojaribiwa wakati wote alikuwa bado
anampenda Mungu kwa kila mapito aliyokuwa anapitishwa na shetani bila ya yeye
kujua. Ayoubu 2:3 inasema, ijapokuwa
shetani alinichochea pasipokuwa na sababu lakini Ayubu alizidi kumpenda Mungu.
Je wewe mapito hayo unayopitia unakuwa bado uko na Mungu au
unakata tamaa kwa mapito hayo. Kumbuka kung’ang’ania ndio mtaji wa kumpendeza
Mungu ajue kuwa kwa mapito anayopitia mwanangu huyu kweli ananipenda. Hapo
lazima Mungu atakuheshimisha kwa yote.
Kitabu cha Danieli 6:1,
lakini tuuangalie mstari ule wa nne (4) unasema, maliwali, madiwani, mawaziri
na viongozi wote katika ufalme ule walimchukia Danieli kwa sababu ya msimamo
wako wa kuwa mtu mwenye haki na mkweli mbele ya bosi wake na mbele za Mungu.
Wakaamua wamuundie sheria ambayo iwapo ataikiuka basi ndipo itakuwa mwisho wa
yeye kuwepo katika uongozi ule.
Lakini Danieli kwa uaminifu wake kwa Mungu hatutetereka yeye
alikaza buti na aliendelea kumtukuza Mungu kwa kelele kubwa ambazo hazikuwa za
siri tena. Ndipo walipo mshitaki kwa sheria yako na akatupwa kwenye tundu la
simba. Lakini kwa upendo wa Mungu aliokuwa nao kwa Danieli hakuliwa na wale
wanyama walikuwa ni marafiki zake. Ndipo yule mfalme aliwaamuru wale wote
walioleta fitina kwake kuhusu Danieli, wachukuliwe wao na familia zao zitupwe
kwenye lile tundu la simba, na kabla hawajafika chini waliraluliwa vipande
vipande na kizazi chao kiliishia hapo.
Je, maadui zako wanataka wamekuandalia mashitaka ya aina gani
mbele ya wakubwa wako, ukiwa kazini, nyumbani, kwenye shughuli zako zozote zile
ambazo unajiendeleza nazo. Kumbuka iwapo unafahamu kuwa kuna watu wamepekela
mashitaka kwa wakuu wako wewe usihofu hata kidogo kwani kuna mtetezi wako
ambaye ni Mkuu kuliko wote nenda mbele zake ukamwambie hao washitaki wako naye
atawashughulikia.
Ili mashitaka uliyoshitakiwa na shetani mbele za Mungu
yaondolewe unafanyaje? Kumbuka kuwa wewe ni mwenye dhambi lakini dhambi hiyo
imesamehewa kwa Damu ya Yesu pale msalabani. Kwa hiyo usije ukajihesabia dhambi
wakati ulisha samehewa.
Kumbuka kuwa kila aliye dhaifu na aseme yeye ni hodari Yoeli 3:10. Iwapo mtu yeyete
atakutamkia kitu kibaya wakati huo huo wewe kanusha kwa kusema kinyume chake,
mgongwa sema mimi ni mwenye afya. Ukiambiwa kuwa wewe ni masikini wewe sema
mimi ni tajiri mbele za Bwana.
No comments:
Post a Comment